Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » BAADHI YA WASHUKIWA WA UJAMBAZI NYUMBANI KWA FINA MANGO WAKAMATWA

BAADHI YA WASHUKIWA WA UJAMBAZI NYUMBANI KWA FINA MANGO WAKAMATWA

tangazo
Baadhi ya washukiwa ujambazi nyumbani kwa mtangazaji wa kipindi cha Makutano cha Magic FM, Fina Mango wamekamatwa.Kwa mujibu wa Fina, majambazi hao wapo kwenye mtandao mkubwa unaofanya vitendo hivyo jijini Dar es Salaam.


Fina Mambo akiwa na familia yake

Kupitia Twitter ameeleza:
Lile kundi la majambazi lilokua likifanya uvamizi wa nyumba zipatazo 7 (kwangu ilikua ya 4) maeneo ya Kawe hadi Mbezi, ilisemekana ni kundi la watu 40 waliosambaa kuanzia Kawe (makao makuu) Mikocheni, Kinondoni mpaka Mbagala, Wameanza kukamatwa.


Polisi Kawe inashikilia watu 7 ambao walikutwa na baadhi ya vitu pamoja na bastola 1 na Gobole 1 matching risasi zilizokutwa maeneo ya tukio.


Waliokamatwa wanaongea na kusema kote walikopeleka mali kuviuza. Ni juhudi za kusifiwa za mmoja wa wahanga maana aliamua kulifatilia swala.


Hili mpaka mwisho wake baada ya kuvamiwa na risasi kupigwa ndani kwake. Kwa ushirikiano na wasamaria wema waliotoa info pamoja na Kawe Police wamekamatwa. Kidogo twaweza lala kwa Amani sasa.


Fina Mambo alivamiwa na majambazi wafikao wanane nyumbani kwake na kupora mali na fedha.
Screenshot 2013-03-25 at 06.49.53
Screenshot 2013-03-25 at 06.50.00
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger