Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » MCHUNGAJI " MASANJA MKANDAMIZAJI" APATA NAFASI YA KUHUBIRI NENO LA MUNGU NCHINI MAREKANI

MCHUNGAJI " MASANJA MKANDAMIZAJI" APATA NAFASI YA KUHUBIRI NENO LA MUNGU NCHINI MAREKANI

tangazo

Mtumishi wa Mungu Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji) ambaye yuko nchini Marekani kwa ziara maalum, atahudumu kwa waumini wa jiji la Washington DC na vitongoji vyake siku ya kesho (Jumapili 07/07/2013) 
 
Bwana  Mgaya ambaye pia hufahamika kama Mchungaji Mtarajiwa  na ambaye amekuwa akifanya huduma ya uhubiri nchini Tanzania, atahubiri katika ibada ya jumapili katika kanisa la THE WAY OF THE CROSS GOSPEL MINISTRIES katika ibada ya kawaida ya kila jumapili ambayo hufanyika kuanzia saa saba kamili mchana mpaka saa tisa kamili alasiri (1:00pm - 3:00pm)

Hii itakuwa ni huduma ya kwanza nchini Marekani kwa Mtumishi huyu ambaye ni Mchungaji msaidizi katika kanisa la EAGT Mito ya Baraka lililopo Kariakoo jimbo la Temeke jijini Dar Es Salaam likiongozwa na Askofu Bruno Mwakibolwa na ameshafanya huduma katika sehemu mbalimbali nchini Tanzania.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger