Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Dr. Slaa na viongozi wengine wa CHADEMA waukana waraka uliosambaa kumhusu Zitto Kabwe....Pamoja na kuukana, Zitto Kabwe adai wahusika ni CHADEMA wenyewe

Dr. Slaa na viongozi wengine wa CHADEMA waukana waraka uliosambaa kumhusu Zitto Kabwe....Pamoja na kuukana, Zitto Kabwe adai wahusika ni CHADEMA wenyewe

tangazo

Maneno haya yametoka kwenye ukurasa wa facebook wa mbunge Zitto Kabwe na yamesemwa na viongozi wa Chadema kama Dr Wilbroad Slaa,Edwin Mtei na Mabere Marando kuhusu waraka uliosambaa kumhusu Zitto Kabwe.

Hii  ni Post ya Zitto Kabwe  aliyoiweka  facebook 
Dr. Willbrod Slaa : ” Hatuna tatizo hata kidogo na Zitto Kabwe. Huyu ni Naibu Katibu Mkuu wetu kama kuna tatizo jambo ambalo ameleta tutamaliza kwa mujibu wa taratibu na tutaendelea na kazi na umoja wetu”
 
” Waraka huo mchafu umeandikwa na viongozi wa CCM na kutoka idara nyeti ya serikali. Chama kitapata taarifa zao na kuanika majina yao na nafasi zao”
 
Edwin Mtei : ” Haya mambo hayatubabaishi tunajua ni uongo uliotungwa ili kutugombanisha. Kesho unaweza kusikia Zitto amehongwa hiki au kile. Keshokutwa ukasikia Slaa amehongwa hiki baadaye Mbowe amefanya hivi lengo kutuvuruga”
 
Mabere Marando:  ”Andishi hili ni feki nimeliangalia andishi lote. Nimejiridhisha kwamba limetengenezwa na watu wasiotakia mema Chadema”
  
Msimamo  wa  Zitto  Kabwe:
Maneno mazuri sana yenye ukweli mtupu. Hata hivyo hekaya hii imesambazwa na wanachama wa CHADEMA na mmoja ni kiongozi wa mkoa na akaweka kwenye blogu yake. Viongozi wengine waka ‘like’ kwenye jamii forums. Hawa wametumwa na usalama na CCM?
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger