Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Magaidi yameendelea kuitesa Kenya: Jana kulikuwa na mapambano kati ya polisi na magaidi ambayo yalizidiwa nguvu na kuuawa

Magaidi yameendelea kuitesa Kenya: Jana kulikuwa na mapambano kati ya polisi na magaidi ambayo yalizidiwa nguvu na kuuawa

tangazo
Taarifa ya  kituo cha TV cha KTN Kenya inasema washukiwa wawili wa Ugaidi kwenye mtaa wa Eastleigh wakidaiwa kuwa miongoni mwa genge lililoshambulia msikiti kwenye mtaa huo December 2012 na kumjeruhi Mbunge wa Kamkunji Yusuf Hassan, wameuwawa asubuhi ya November 13 2013.
 
Mtaa huo ambao unaaminika kuwa chimbuko la Wanamgambo wa kundi la kigaidi la Al Shabaab ambapo mwaka huo wa 2012 washukiwa hao walifanikiwa kutoroka, mmoja kwa gari na mwingine kwa miguu umeshuhudia washukiwa hao wakiuwawa na Polisi waliokua wakiwasaka kwa muda kabla ya kuwapata.

Walioshuhudia kisa hiki kipya wanasema Polisi walitaka wajisalimishe lakini wakagoma hivyo wakaamua kuwaua kwa risasi kwenye mtaa huu huu wenye Wakimbizi laki sita kutoka Somalia ambao hawajasajiliwa huku hiyo ikisemekana kuwa njia rahisi kwa Wanamgambo wa Al Shabaab kuingia Kenya.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger