Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Muimbaji na Mtangazaji wa kipindi cha taarab cha Passion FM, Nyawana Fundikira afariki dunia

Muimbaji na Mtangazaji wa kipindi cha taarab cha Passion FM, Nyawana Fundikira afariki dunia

tangazo

Muimbaji na mtangazaji wa kipindi cha taarab cha Passion FM ‘Ambaa na Mwambao’, Nyawana ‘Matashtiti’ Fundikira amefariki dunia  jana.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mume wake, Nyawana amefariki kwa ugonjwa wa Malaria na mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwake Mwananyamala, Dar es Salaam.
 
Pamoja na utangazaji, Nyawana alikuwa muimbaji wa taarab pia na alijiunga na Tanzania Moto Modern Taarab, maarufu kama T-Moto pamoja na KINGS MODERN TAARABU.

 Aliwahi pia kuwa mtangazaji wa Voice of Tabora na nyimbo alizorekodi ni pamoja na ‘Nipo Kamili’ na ‘Umesharoga Wangapi’.

Nyawana aliyewahi kuwa Miss Tabora mwaka 1996, ameacha mume na watoto wawili. Alizaliwa mwaka 1977 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kupata elimu yake msingi kwenye shule ya Zanaki huku sekondari akisoma Masjid Quba na Al Haramain.

Baada ya hapo alisomea Uhazili kabla ya kumaliza na kusomea masomo ya Uandishi wa Habari na Utangazaji, ambapo pia alishiriki shindano la urembo na kunyakua taji la Miss Tabora, mwaka 1996.

Source: Bongo5
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger